Recent comments

Breaking News

Hii ni interview ya kwanza ya mwigizaji Kajala, yani ndio kwa mara ya kwanza kahojiwa kwenye chombo cha habari (Exclusive on bongohitz1.blogspot.com)


kajala
Hii ni interview ya kwanza ya mwigizaji Kajala, yani ndio kwa mara ya kwanza kahojiwa kwenye chombo cha habari (Exclusive on bongohitz1.blogspot.com) baada ya kumiliki headlines kwa ishu zake tatu ambazo ni kuchukua mume wa mtu, kudaiwa kukamatwa na dawa za kulevya na safari yake kwenda China.

Yafuatayo ni maswali ya bongohitz1.blogspot.com nyumbani kwake Dar es salaam.
Bongo Hitz1 : Ni kweli kuhusu hii ya mume wa mtu?
Kajala: Hapana, niliambiwa mtu wa kwanza kuandika hii alikua mtu wa blog ndio magazeti na mitandao mingine ikafata ila sio kweli… sikufatilia manake ukweli naujua mwenyewe, niliumia na hata mama yangu aliumia na aliniuliza.
Kwenda club au kukutana na mtu na kupiga nae picha sio kwamba umeiba mume wa mtu, huyo dada kama kweli yule angekua mume wake angenifata manake haya kuniona hivi hajawahi… yeye yuko Hongkong mi niko China ananiambia nimeiba mume wake…. huyu Mwanaume anaishi hukohuko, China nilikwenda mwenyewe na wala sio kwamba nimetoka nae Tanzania.
Bongo Hitz1: Siku unapigwa picha ukiwa na huyu mwanaume Club ulikua unajua unachukuliwa picha?
kajala mume wa mtu
Kajala: Siku hii ilikua ni birthday ya mwenye club, mimi sikujua kama napigwa picha ndio zikasambazwa kwenye mtandao, wale wadada wamezichukua huko ndio wakaanza kunitukana.

Bongo Hitz1 : Vipi kuhusu hii iliyoandikwa ya wewe kukamatwa na dawa za kulevya Airport?
Kajala: Sio kweli manake hata dawa zenyewe za kulevya sijui zilivyo zaidi ya kuziona tu kwenye TV, sasa hivi kila staa akipita kwenye uwanja wa ndege Dar ni lazima asachiwe sana kwa sababu wanasema ‘nyinyi mastaa mnatuharibia sana kazi’ kwa hiyo lazima wakuweke pembeni kukukagua.
Bongo Hitz1 : Safari yako ya China ilihusu nini?
Kajala: Nilikwenda kufanya shopping tu sababu ya movie yangu naanza kushoot January 2014 kwa hiyo nikaenda kununua vitu vya kuvaa, sio Camera wala vifaa… ni nguo tu, shopping inazidi milioni kumi.
kajala 12
Bongo Hitz1: Inaweza kutokea siku moja tukasikia Kajala kaolewa?

Kajala: Ndoa yangu ni ya kanisani ila sijui kama nitaruhusiwa kuolewa tena kwahiyo namsubiria labda mume wangu akitoka Jela, sina mpango wowote wa kuolewa kwa sasa japo napata usumbufu ila nawaambia tu mume wangu yuko jela, huwa namtembelea kila weekend…. kukaa kwake jela kumeniathiri sana, tulikaa kwenye ndoa miezi sita tu kabla ya misukosuko kuanza, nilikua nampango wa kupata mtoto mwingine wa pili ili niwe nimemaliza ila sasa hivi siwezi kuzaa, nimekaa tu namsubiria…..

No comments