Recent comments

Breaking News

Breaking: Taarifa kamili kuhusu boti iliyotupa watu 10 baharini ikitokea Pemba.


breaking
Boti ya Kilimanjaro II ikitokea Pemba kuelekea Unguja imepigwa na dhoruba leo Jan 5 2014 kwenye saa nne asubuhi na kuponea kuzama ilipokua kwenye eneo hatari la Nungwi ambapo ilizama kidogo mbele na kunyanyuka hivyo watu wa mbele wote wakaachwa lakini pamoja na kuwatupa hao watu kwenye maji Nahodha akafanya uamuzi mwingine mgumu.


Aliona akisimama ili kuwaokoa wale watu boti yote ingezama pale hivyo akaamua kuendelea na safari lakini kabla ya kuondoka watu kadhaa ndani ya boti wakajitolea kuwatupia life jacket wale waliotupwa kwenye maji ambapo shuhuda anasema kama mtu hajui kuogelea anaweza kupoteza maisha kwa sababu hawakua wamejiandaa kwenye tukio hili la ghafla na sio wote wamepata vifaa hivyo vya kujiokoa.
Shuhuda mmoja anasema ‘yani boti ilizama ghafla mbele hivyo watu wakatupwa kwenye maji kwenye hii sehemu ambayo kuna mkondo wa maji, upepo ulikua mkali sana yani unaona watu wanajaribu kujiokoa mabegi na vitu vingine vinaonekana juu ya maji’
Hali ilivyo ndani ya boti ambayo imeendelea na safari ni watu kujawa na huzuni na wengine wamebaki wanalia tu.
bahari
Boti hiyo ina zaidi ya abiria 600 na chanzo ni upepo mkali ambapo mmoja wa abiria aliehojiwa na Clouds FM amesema toka mwanzo alikua na wasiwasi na safari ya leo manake bahari haijatulia kabisa ambapo kwa sasa abiria wote wamepewa life jacket.

Bongo Hitz1 wakishirikiana na Millardayo inaendelea kufatilia kwa undani taarifa hizi endelea kuwa karibu nasi.
Bonyeza play kusikiliza mashuhuda wakielezea hii ajali hapa chini.


No comments