MH.ZITO KABWE (KIGOMA-CHADEMA)
Kambi rasmi ya upinzani bungeni
imewasilisha bajeti mbadala ya kambi hiyo kwa mwaka wa fedha 2012/2013
na kuitaka serikali kuwa makini katika kukopa nje ya nchi kutokana na
kukua kwa kasi kwa deni la taifa na kupendekeza pia magari ya kifahari
ya serikali yapigwe mnada ili kupunguza matumizi ya mafuta.
Pamoja na hizo ishu kambi hiyo
imeitaka serikali kuainisha njia za kudhibiti mfumuko wa bei
unaowaongezea mzigo wananchi na kuwaongezea mishahara walimu, madaktari
na wauguzi kwa asilimia 50 huku ikiweka mpango wa kuanza kuwalipa
pensheni wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60.
Mbunge wa Kigoma Kaskazini kwa
ruhusa ya Chadema Zitto Kabwe ambae pia ni waziri kivuli wa fedha
amesema “swala ni kwamba tunakopa ili kufanya nini? bajeti ya mwaka
2012/2013 inayopendekezwa inaonyesha kwamba serikali itakusanya trilioni
8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia shilingi trilioni 10.6 kama
matumizi ya kawaida, ni dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali
inachukua sasa itakwenda kwenye matumizi ya kawaida, hatutaki mikopo kwa
ajili ya matumizi ya posho”
Kabwe amekamilisha kauli yake
akikaririwa akisema “tuchukue mikopo kuwekeza kwenye miradi itakayokuza
uchumi na kuzalisha kodi zaidi, kuiacha serikali kuendelea kukopa bila
mpango ni kuliweka taifa rehani, hatuwezi kukubali wazee wetu waishi
maisha yao waishi maisha yetu na wakope maisha ya watoto wetu”
Wabunge mbalimbali walichangia
bungeni Dodoma June 18 2012 na kulalamikia kuongezeka kwa deni la taifa,
usimamizi mbaya wa rasilimali za nchi na ugumu wa maisha kwa mtanzania
na wengine wakakataa kuiunga mkono bajeti hiyo.
No comments:
Post a Comment