MOYO WA FLAVIANA MATATA KWENYE KUMBUKUMBU YA MV BUKOBA.
 
Mwanamitindo mtanzania Flaviana
 Matata ametoa life Jackets mia tano (500) na kuzikabidhi kwa mamlaka ya
 bandari Mwanza (TPA) kama kumbukumbu ya miaka kumi na sita ya ajali ya 
meli ya MV BUKOBA.
Flaviana amesema “nimetoa hizo 
life Jackets kwa ziwa Victoria ambapo ajali hiyo ndipo ilipotokea ambapo
 mama yangu alikua mmoja wa waliofariki dunia”
Flaviana Matata mwenye makazi 
yake London U.K na New York Marekani anakofanya kazi, amesema alitoka na
 hizo Life Jackets nje ya nchi baada ya kuzioda kiwandani na angependa 
watanzania wenye uwezo wa kufanya hivyo wafanye pia, yeye ameshafungua 
milango”
No comments