DIAMOND PLATNUM AINGIA MKATABA NA I-VIEW MEDIA
Mkurugenzi wa kampuni ya I-View Studios, Raqey Mohammed akibadilishana
mkataba na Msanii Diamond Platnumz baada ya kusaini. Wanaoshuhudia ni
Mwanasheria wa Diamond, Paul Mgaya, Mwanasheria wa I-View Dr. Peter
Aringo na Mkurugenzi wa One Touch Solutions, Petter Mwendapole.
Mkurugenzi wa Kampuni ya I-View Studios, Raqey Mohammed ( kushoto) na
msanii Diamond Platnumz wakisaini mkataba wa kufanya kazi pamoja. Wanaoshuhudia ni
Mwanasheria wa Diamond, Paul Mgaya, Mwanasheria wa I-View Dr. Peter
Aringo na Mkurugenzi wa One Touch Solutions, Petter Mwendapole
MSANII wa kimataifa wa Tanzania, Naseeb Abdul
‘Diamond Platnumz’ ameingia mkataba na kampuni ya I-View Studios ya ili
wasimamie kazi zote kwa muda wa miaka miwili.
Mkurugenzi wa kampuni ya One Touch Solution ya
mjini Dar es Salaam, Petter Mwendapole amesema I-View itasimamia mikataba yote
ya kazi zote za msanii huyo na yeyote atakayetaka kufanya kazi na Diamond kwa
sasa itabidi awasiliane I-View.
No comments