Recent comments

Breaking News

Sir Andy Chande Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons


Sir Andy Chande
*Nimepata kutambua umuhimu wa mafunzo ya Freemason katika kujenga hisia za utuwema na ukweli kwake mtu wenyewe na kw abinadamu wenzake. Moyo wangu mawazo yangu na roho yangu, vyote vimeimarika kutokana na kushiriki kwangu katika Freemason

*Mwaka 1972 nikachukua hatua yangu ya kwanza kuelekea kwenye madaraka makubwa zaidi katika Freemason nilipochaguliwa Afrisa Mkuu wa Wilaya wa kufanya kazi na Makao makuu ya Freemason ya Mkoa kule Nairobi ambao wakati ule ulikuwa unasimamia makambi kiasi cha ishirini na manane katika Afrika nzima

*Freemason Tanzania wamesaidia kituo cha watu wenye ukoma cha kindiwi wilayani Utete; Kituo cha watoto cha Mama Theresa; shule  ya Vipofu ya Pongwe, mkoani Tanga; Kituo cha yatima cha Arusha, Hospitali ya Mnazi mmoja kula Zanzibar; na Shule ya Viziwi ya Buguruni.


Tangu miaka hiyo ya 1920 idadi ya  vikundi vya Mason nchini Tanzania na  Afrika Mashariki kwa ujumla imeendelea kuongezeka. Ogezeko  kama hilo hilo limejidhihirisha katika Asia, Marekani ya  kusini, na baadaye Ulaya ya Mashariki, baada ya kipindi kile cha kuingia kwa ukomanisti lakini kwingine kote hasa Ulaya ya Magharibi, Amerika ya  Kusini na Australia, idadi ya Wanachama wa Mason wamekuwa wakipungua polepole na kuacha pengo kubwa duniani kutoka milioni saba waliokuweko wakati wa vita kuu ya kwanza hadi kufikia milioni tano tu.
 
Sir Andy Chande kulia akiwa na Rais Benjamin Mkapa


Sir Andy Chande akiwa na wenzake wakipanda Miti jijini Tanga kama moja ya shughuli zao za kijamii

Hivyo hiyo ndiyo dunia niliyoitumbukia mwaka 1954, na ikawa sehemu muhimu ya maisha yangu kuanzia hapo. Katika kipindi hicho nimepata bahati ya kushuhudia kujitolea kwa Wanachama wa Freemason katika kuwasaidia wenye shida ndani ya Afrika Mashariki na hata nje ya hapo. Nimepata kutambua umuhimu wa mafunzo ya Freemason katika kujenga hisia za utuwema na ukweli kwake mtu wenyewe na kw abinadamu wenzake. Moyo wangu mawazo yangu na roho yangu, vyote vimeimarika kutokana na kushiriki kwangu katika Freemason; na kuimarika huko kunatofautiana kabisa na hisia zinazotangazwa katika magazeti mashuhuri ya nchi za magaribi. Kuwasaidia wenzetu kuwasaidia wengine ndiyo misingi niliyojifunza katika miaka yangu mingi ndani ya Freemason.

No comments