HII NDIO STORI KAMILI KUHUSU MWANAMKE ALIYECHINJWA KAMA KUKU NA MUME WAKE
VILIO vilitawala Kata ya Nyahanga wilayani hapa wakati wa kuuaga 
mwili wa binti Jessica Elialinga (19) aliyeuawa kinyama kwa kuchinjwa 
kama kuku na mpenzi wake, Musa Petro (27) mkazi wa Shunu kwa sababu 
zinazodaiwa ni wivu wa kimapenzi.
Kitendo hicho kilifanyika katika banda la mbuzi lililopo nyumbani kwa kijana huyo ambaye baada ya kutekeleza mauaji na yeye alifanya jaribio la kutaka kujitoa roho kwa kisu.
Akisimulia juu ya tukio hilo, rafiki wa karibu wa Musa ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya usalama, alisema wiki moja kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa huyo alikuwa akiwatangazia jamaa zake kwamba ana dhamira ya kumuua binti huyo kufuatia kubaini kuwa anamsaliti kimapenzi.
“Alisema anataka kufanya hivyo kwa sababu amekuwa akitumia gharama kubwa kwa mpenzi wake huyo tangu walipoanza uhusiano, msichana akiwa kidato cha pili, lakini anatoka kimapenzi na mwanaume mwingine,” alisema rafiki huyo.
Hata hivyo, inadaiwa baada ya mtafaruku wa usaliti, wawili hao walipatana na kuendelea na mapenzi, lakini baada ya mwanafunzi huyo kuhitimu kidato cha nne alibadilika ambapo mwanaume alisikia kuwa tayari ana mwanaume mwingine kutoka jijini Mwanza ambaye walikubaliana kufunga pingu za maisha baada ya kumaliza masomo.
Jessica Elialinga baada ya kuchinjwa.
Tukio hilo lililoibua simanzi kubwa kutokana na marehemu kuhitimu 
Kidato cha Nne katika Shule ya Sekondari ya Kata ya Nyihogo, Kahama 
mwaka jana, lilijiri saa 12:45 Februari 6, mwaka huu.
Kitendo hicho kilifanyika katika banda la mbuzi lililopo nyumbani kwa kijana huyo ambaye baada ya kutekeleza mauaji na yeye alifanya jaribio la kutaka kujitoa roho kwa kisu.
Akisimulia juu ya tukio hilo, rafiki wa karibu wa Musa ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya usalama, alisema wiki moja kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa huyo alikuwa akiwatangazia jamaa zake kwamba ana dhamira ya kumuua binti huyo kufuatia kubaini kuwa anamsaliti kimapenzi.
Muuaji Musa Petro.
 “Unajua Musa anafanya kazi ya kuchuna ngozi za wanyama machinjio ya 
Wilaya ya Kahama, alitutangazia dhamira yake hiyo, lakini tulichukulia 
kauli yake kama mzaha.
“Alisema anataka kufanya hivyo kwa sababu amekuwa akitumia gharama kubwa kwa mpenzi wake huyo tangu walipoanza uhusiano, msichana akiwa kidato cha pili, lakini anatoka kimapenzi na mwanaume mwingine,” alisema rafiki huyo.
Hata hivyo, inadaiwa baada ya mtafaruku wa usaliti, wawili hao walipatana na kuendelea na mapenzi, lakini baada ya mwanafunzi huyo kuhitimu kidato cha nne alibadilika ambapo mwanaume alisikia kuwa tayari ana mwanaume mwingine kutoka jijini Mwanza ambaye walikubaliana kufunga pingu za maisha baada ya kumaliza masomo.
Enzi za uhai wake 


 
No comments