Recent comments

Breaking News

BREAKING NEWS:- VURUGU ZA MBAGALA ZAHAMIA MJINI, WAISLAMU WAANDAMANA NA KUZINGILA KITUO CHA POLISI



Habari zilizotufia hivi punde kutoka katika chanzo cetu cha habari ni kwamba kuna vurugu zinazoendelea sasa maeneo ya mjini, stesheni katika kituo cha polisi, ambapo waislamu wameandamana na kukizingila kabisa kituo hicho cha polisi na kutaka kuachiwa kwa Sheikh wao, hii ni baada ya kukamatwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda (Katibu wa taasisi za jumuiya ya Kiislamu) aliyekuwa akiitaka polisi iwaachie waislam waliokamatwa katika vurugu za Mbagala baada ya kuchoma makanisa kadhaa huko Zakiem. Mpaka sasa maduka yote ya wafanyabiashara huko mjini yamefungwa na hakuna huduma au shughuli yoyote inayoendelea kwa sasa.
Polisi wamedhibiti katika mitaa kwa kutumia mabomu ya machozi na magari yanayotoa maji yenye kuwasha katika hali ya kuleta amani na kutaka kuwatanya waandamaji hao kwa kutuliza ghasia, mpaka serikali itakapotia shauri lake juu ya suala hili, ili amani iwepo.

Tutaendelea kuwajuza yatakayojiri.

Mmoja wa wafuasi wa kikundi cha waislamu wenye imani kali akidhibitiwa na polisi mara baada ya kukamatwa leo katika kituo kikuu cha polisi Kati wakijaribu kuandamana ili kushinikiza kiongozi wao Katibu wa Taasisi za Kiislamu Shekh Ponda Issa Ponda kuachiwa na jeshi la polisi mara baada ya kukamatwa jijini Dar es salaam kwa kudaiwa kusababisha vurugujijini Dar es salaam.
Mwandamanaji mwingine akipelekwa katika kituo kikuu cha polisi kati jijini Dar es salaam leo mchana mara baada ya kukamatwa akiandamana.



No comments