Sir Andy Chande Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons
![]() |
Sir Andy Chande |
*Nimepata
kutambua umuhimu wa mafunzo ya Freemason katika kujenga hisia za
utuwema na ukweli kwake mtu wenyewe na kw abinadamu wenzake. Moyo wangu
mawazo yangu na roho yangu, vyote vimeimarika kutokana na kushiriki
kwangu katika Freemason
*Mwaka
1972 nikachukua hatua yangu ya kwanza kuelekea kwenye madaraka makubwa
zaidi katika Freemason nilipochaguliwa Afrisa Mkuu wa Wilaya wa
kufanya kazi na Makao makuu ya Freemason ya Mkoa kule Nairobi ambao
wakati ule ulikuwa unasimamia makambi kiasi cha ishirini na manane
katika Afrika nzima
*Freemason Tanzania wamesaidia kituo cha watu wenye ukoma cha kindiwi wilayani Utete; Kituo cha watoto cha Mama Theresa; shule ya
Vipofu ya Pongwe, mkoani Tanga; Kituo cha yatima cha Arusha, Hospitali
ya Mnazi mmoja kula Zanzibar; na Shule ya Viziwi ya Buguruni.
Tangu miaka hiyo ya 1920 idadi ya vikundi vya Mason nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla imeendelea kuongezeka. Ogezeko kama hilo hilo limejidhihirisha katika Asia, Marekani ya kusini,
na baadaye Ulaya ya Mashariki, baada ya kipindi kile cha kuingia kwa
ukomanisti lakini kwingine kote hasa Ulaya ya Magharibi, Amerika ya Kusini
na Australia, idadi ya Wanachama wa Mason wamekuwa wakipungua polepole
na kuacha pengo kubwa duniani kutoka milioni saba waliokuweko wakati
wa vita kuu ya kwanza hadi kufikia milioni tano tu.
Sir Andy Chande kulia akiwa na Rais Benjamin Mkapa
Sir Andy Chande akiwa na wenzake wakipanda Miti jijini Tanga kama moja ya shughuli zao za kijamii |
Hivyo
hiyo ndiyo dunia niliyoitumbukia mwaka 1954, na ikawa sehemu muhimu ya
maisha yangu kuanzia hapo. Katika kipindi hicho nimepata bahati ya
kushuhudia kujitolea kwa Wanachama wa Freemason katika kuwasaidia wenye
shida ndani ya Afrika Mashariki na hata nje ya hapo. Nimepata kutambua
umuhimu wa mafunzo ya Freemason katika kujenga hisia za utuwema na
ukweli kwake mtu wenyewe na kw abinadamu wenzake. Moyo wangu mawazo
yangu na roho yangu, vyote vimeimarika kutokana na kushiriki kwangu
katika Freemason; na kuimarika huko kunatofautiana kabisa na hisia
zinazotangazwa katika magazeti mashuhuri ya nchi za magaribi. Kuwasaidia
wenzetu kuwasaidia wengine ndiyo misingi niliyojifunza katika miaka
yangu mingi ndani ya Freemason.
No comments