Recent comments

Breaking News

IJUE TANZANIA YAKO NCHI YENYE UDONGO WENYE DHAMBI


Natumaini sote ni wazima katika harakati za ujenzi wa taifa letu, ambapo wanasiasa wachache wanaoficha maovu yao nyuma ya mazabao wanaliita ni taifa changa. Kwa mtazamo wangu Tanzania si taifa changa bali Tanzania ni taifa lilofunikwa na udongo wenye dhambi.Dhambi ambazo zinatesa wale wasiokuwa nacho kuwa chini ya waliokuwa navyo na kuwa watumwa ndani ya nchi yao.Hii ni dhambi ambayo inahitaji makemeo ya hali na mali ili kupisha uongozi safi.
Ikumbukwe kuwa Desemba 09’1961 Tanzania ilipata uhuru wake kutoka kwa Muingereza, ambaye alikuwa mtawala baada ya ukoloni wa Ujerumani. Ambapo Hayati Mwl.julius K.Nyerere ndiye aliyetawazwa kuiongoza Tanganyika  kama waziri mkuu mpaka mwaka 1962 ambapo ndipo Tanganyika ilipata Jamhuri na kuwa na raisi wake. Toka mwaka 1961 mpaka miaka ya 1970 Tanganyika ilikuwa inatumia katiba iliyoachwa na muingereza. Lakini mwazoni mwa miaka ya 1970 Tanganyika baada ya kuungana na Zanzibar mwaka 1964, ilisahihisha na kurekebisha pasipo kubadilisha katiba hiyo. Japokuwa inasemekana kwamba ilibadilishwa kwa mitazamo isiyo wazi. Hii ina maana ya kwamba haikujali Demokrasia ya kweli kwa raia wake, Lakini hakuwepo mtetezi wala aliyedhani juu ya hili.
Vuguvugu la uongozi bora juu ya kuwakandamiza wahujumu uchumi liliendelea wazi serikalini katika uongozi wa awamu ya kwanza. Hii ilipelekea Hayati Mwl.Julius K. Nyerere kuleta azimio la Arusha mnamo mwaka 1967. Ambapo azimio  hilo lilikuwa likitetea sera ya uongozi bora,ambapo Mwalimu alikemea baadhi ya mambo ili kufanya Tanzania kuwa na tija katika uchumi wake. Hii ilikuwa ni kuhakikisha kuw hakuna atakayethubutu kufanya uhujumu uchumi katika serikali yake. Na pia kuhimiza baadhi ya mambo katika serikali yake ikiwemo siasa ya ujamaa.
Lakini Azimio halikudumu, lilikandamizwa na kupigwa chini na wajanja wachache ambao walihitaji kujinufahisha. Tanzania haikufahulu katika hilo hivyo kufanya raia wake kubaki masikini na kuzidi kuwa wanyonge ndani ya taifa huru bandia.
Mwaka 1992, Mwalimu alileta hoja ya mfumo wa vyama vingi, ambapo kura za maoni zilipopigwa Watanzania baadhi hawakutaka mfumo huu, lakini Mwalimu akataka mfumo huo upitishwe na mchakato wa usajili wa vyama vya siasa uanze mara moja.Wapo ambao wanasema kwamba hii ilikuwa ni hekima ya Mwalimu,lakini wachunguzi na wataalam wa siasa wanadai kwamba hii ilitokana na nchi zilizoendelea huko ulaya pamoja na benki ya dunia kutaka nchi zote za Afrika ziwe ndani ya mfumo wa vyama vingi ili kupisha demokrasia ya kweli kwa nchi hizo.



No comments